Mfano na Muundo wa Barua ya Maombi ya Kazi Kujiunga Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)

Mfano na Muundo wa Barua ya Maombi ya Kujiunga Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)

Je Unataka Kutuma Maombi ya Nafasi za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Unakwama katika uandishi wa Barua ya kutuma Maombi yako?Usikonde tumekuandalia hii makala kuyafanya maisha uwa rahisi tumeelezea muundo wa namna Barua inavyotakiwa kuwa pia Tumekuwekea Barua ya mfano.

Vitu Muhimu vya Kuzingatia  katika kuandika Barua ya Kuomba kujiunga JWTZ

  1. Anwani ya Mwombaji
  2. Tarehe
  3. Anwani ya Kupokea
  4. YAH: Maombi ya Nafasi ya Kujiunga na JWTZ
  5. Utangulizi
  6. Maelezo Binafsi na Sifa
  7. Hitimisho
  8. Jina na Sahihi ya Mwombaji

Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)

 

  1. Anwani ya Mwombaji
  2. Tarehe
  3. Anwani ya Kupokea
  4. YAH: Maombi ya Nafasi ya Kujiunga na JWTZ
  5. Utangulizi
  6. Maelezo Binafsi na Sifa
  7. Hitimisho
  8. Jina na Sahihi ya Mwombaji

Mfano wa Barua

[Anwani yako]

[Tarehe]

Mkuu wa Utumishi Jeshini

Makao Makuu ya Jeshi

Sanduku la Posta 194,

DODOMA, TANZANIA.

YAH: MAOMBI YA NAFASI ZA KAZI JWTZ 2024

Ndugu,

Kwa heshima na taadhima, mimi [Jina Lako], raia wa Tanzania mwenye kitambulisho cha Taifa au namba ya NIDA [Namba yako ya NIDA], naandika kuomba nafasi ya kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa mwaka 2024 kama ilivyotangazwa.

Nina elimu ya kidato cha [nne/sita] na umri wa miaka [umri wako], ambapo napenda kujiunga na JWTZ ili kulitumikia taifa langu kwa moyo mkunjufu. Nina sifa zote zinazohitajika, kama ifuatavyo:

  1. Mimi ni raia wa Tanzania.
  2. Umri wangu hauzidi miaka 25.
  3. Nina afya njema na akili timamu.
  4. Nina tabia na nidhamu nzuri, sijawahi kupatikana na hatia ya jinai wala kuhukumiwa kifungo.
  5. Sijawahi kutumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo, au Kikosi Maalumu cha kuzuia Magendo.
  6. Nimehitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa mkataba wa kujitolea kwa miaka miwili na ninayo cheti husika.
SOMA HII :  Orodha ya Vyuo vya Afya Mkoani Dodoma (Serikali na Binafsi)

Ninatumaini kwamba maombi yangu yatapata nafasi ya kujadiliwa na hatimaye kupitishwa. Nafurahia kujiunga na JWTZ ili kujenga mustakabali mzuri kwa taifa langu na kwa dunia kwa ujumla.

Nimeambatanisha nyaraka zote muhimu kama zilivyoainishwa kwenye tangazo:

  1. Nakala ya kitambulisho cha Taifa/NIDA.
  2. Nakala ya cheti cha kuzaliwa.
  3. Nakala za vyeti vya shule.
  4. Nakala ya cheti cha JKT.
  5. Nambari ya simu ya mkononi: [Namba yako ya simu].

Nina imani kuwa nyaraka hizi zitakidhi mahitaji yote na kutoa mwanga wa sifa zangu. Niko tayari kufika kwa usaili na majaribio mengineyo kama itakavyohitajika.

Ninaomba nafasi hii kwa unyenyekevu na matumaini makubwa. Natanguliza shukrani zangu kwa muda na fursa ya kujadili maombi yangu.

Wako kwa uaminifu,

[Jina Lako]
[Anwani yako]
[Namba ya Simu]
[Barua pepe yako, ikiwa nayo]

 

Fahamu Jinsi ya kuandika Barua ya Maombi ya kazi JWTZ (Jeshi la Wananchi Tanzania ,Tumekuwekea Muundo na mfano wa Barua

Vidokezo Muhimu

  • Anwani: Hakikisha umeandika anwani yako kamili na sahihi.
  • Tarehe: Andika tarehe ya kuandika barua.
  • YAH: Eleza kwa ufupi lengo la barua yako.
  • Utangulizi: Eleza jinsi ulivyopata taarifa ya nafasi hiyo.
  • Maelezo Binafsi na Sifa: Toa maelezo ya elimu yako, sifa na uzoefu unaohusiana na nafasi unayoomba.
  • Hitimisho: Eleza matumaini yako na shukrani zako kwa kuzingatia maombi yako.

Muongozo wa Video Jinsi Ya Kuandika Barua Nzuri Ya Kuomba Nafasi Za Jeshi (JWTZ)

About Burhoney 4807 Articles
Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati