Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Moshi Jonathan Kabengwe ameeleza kuwa TRA Wamepokea Maombi ya ajira 135,027 Baada ya Mchujo Walipata Watahiniwa Wallioidhi Vigezo 112,952 ambao wataitwa Kwenye Usaili kuchuana kugombania Nafasi 1,596 Za Ajira zilizotangazwa Ambapo usaili utafanyika Mikoa Mbalimbali kutegemeana na mtahiniwa alipoomba .
Soma Hii :Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili TRA 2025 PDF Download
Vituo vya Kufanyia Usaili TRA Mamlaka ya Mapato Tanzania Interview Venue 2025
Bw. Kabengwe amesema usaili huo utafanyika kwenye Mikoa 8 na Zanzibar ambayo ni
1. Dar es Salaam ambayo itahusisha waombaji kutoka Dar es Salaam na
Pwani.
2. Zanzibar ambayo itahusisha waombaji kutoka Unguja na Pemba
3. Arusha ambayo itahusisha waombaji kutoka Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga
4. Dodoma ambayo itahusisha waombaji kutoka Morogoro, Dodoma, Singida, Iringa na Tabora
5. Mtwara ambayo itahusisha waombaji kutoka Mtwara, Lindi na Ruvuma
6. Mbeya ambayo itahusisha waombaji kutoka Mbeya, Songwe na Rukwa
7. Mwanza ambayo itahusisha waombaji kutoka Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu
8. Kagera ambayo itahusisha waombaji kutoka Kagera na Geita na
9. Kigoma ambayo itahusisha waombaji kutoka Kigoma na Katavi.