Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Ametangaza Nafasi Mpya za Ajira za kujiunga na Jeshi la Polisi kwa Mwaka 2025 Vijana wa Kitanzania wazalendo na wenye sifa na Vigezo kulitumikia kwa weredi Jeshi la polisi wanakaribishwa Kutuma Maombi.
Taarifa ya Ajira za Jeshi la Polisi
Muajiri : Jeshi la Polisi
Tarehe ya mwisho Kupokea Maombi : 04/04/2025
Nchi : Tanzania
Muhtasari Kuhusu Jeshi la Polisi Tanzania
Jeshi la Polisi la Tanzania ni moja ya vyombo muhimu vya usalama nchini, linalohusika na kuhakikisha amani, utulivu, na usalama kwa wananchi.
Madhumuni na Majukumu ya Jeshi la Polisi
- Kuhakikisha usalama wa raia na mali zao: Polisi wanawajibika kudumisha utulivu na kuzuia uhalifu katika jamii.
- Kufanya uchunguzi wa uhalifu: Polisi wana jukumu la kuchunguza matukio ya uhalifu na kukusanya ushahidi ili kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria.
- Kulinda sheria na amri: Polisi ni chombo cha kutekeleza sheria na amri za serikali.
- Kusaidia na kuelimisha jamii kuhusu masuala ya usalama: Polisi pia hutoa elimu kuhusu umuhimu wa usalama na sheria.
SIFA ZA MUOMBAJI
- Awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.
- Wazazi wake wawe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.
- Awe amehitimu kidato cha nne au sita kuanzia mwaka 2019 hadi 2024.
- Kwa waombaji wa kidato cha nne na sita pamoja na wenye Astashahada wawe na umri kuanzia miaka 18 hadi 25.
- Kwa waombaji wa kidato cha nne wawe na ufaulu wa daraja la kwanza mpaka la nne (Division I-
- Kwa waombaji wenye ufaulu wa daraja la nne (Division IV) wawe na ufaulu wa alama (Points) 26 hadi 28.
- Kwa waombaji wa kidato cha sita wawe na ufaulu wa daraja la kwanza mpaka la tatu (Division I – III)
- Wahitimu wa Shahada na Stashahada wawe na umri kuanzia miaka 18 hadi 30.
- Awe na urefu usiopungua futi tano na inchi nane (5’8″) kwa wanaume, na futi tano inchi nne (5’4″) kwa wanawake.
- Awe na kitambulisho cha taifa au namba ya utambulisho kutoka mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA).
- Awe na uwezo wa kuongea lugha ya Kiswahili na Kingereza kwa ufasaha.
- Awe na afya njema kimwili na kiakili iliyothibitishwa na daktari wa Serikali.
- Awe hajaoa/kuolewa au kuwa na mtoto/watoto.
- Awe hajawahi kutumia dawa za kulevya za aina yoyote.
- Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya awali ya taaluma ya Polisi.
- Awe hajaajiriwa au hajawahi kuajiriwa na taasisi nyingine ya Serikali.
- Awe tayari kufanya kazi za Polisi mahali popote Tanzania.
- Awe tayari kujigharamia katika hatua zote za usaili endapo ataitwa kwenye usaili.
- Asiwe na alama za kuchorwa mwilini (tattoo).
- Asiwe na kumbukumbu za uhalifu.
Kwa waombaji wenye elimu ya kiwango cha Shahada (NTA level 8), Stashahada (NTA level 6) na Astashahada (NTA Level 5 au NVA Level 3) wanatakiwa wawe na fani zilizoainishwa kwenye tangazo hili.
Nafasi Mpya za Kazi Kutoka Jeshi la Polisi Tanzania Machi 2025.
Imetolewa na:
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania,
Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,
S.L.P 961,
DODOMA.
20/03/2025
Soma Hii : Sifa na Vigezo vya Kujiunga na Jeshi La Polisi Tanzania
FANI ZINAZOTAKIWA KWA KILA NGAZI YA ELIMU (TANZANIA BARA)

UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
Waombaji wote wanatakiwa waandike barua za maombi wao wenyewe kwa mkono (Handwriting) bila kusahau namba za simu na watumie anuani ya Mkuu wa Jeshi la Polisi S.L.P 961 DODOMA.
Soma Hii : Mfano wa Barua ya Maombi ya Kujiunga na Jeshi la Polisi
Barua hiyo iambatishwe kwenye maombi ikiwa kwenye mfumo wa ‘pdf.
Waombaji wote wafanye maombi yao kupitia kwenye mfumo wa Ajira wa Polisi (TANZANIA POLICE FORCE RECRUITMENT PORTAL) unaopatikana kwenye kiunganishi (link) cha tovuti ya Jeshi la Polisi (https://ajira.tpf.go.tz).
Soma Muongozo :Jinsi Ya Kutuma Maombi Ajira Za Jeshi La Polisi Online Hatua kwa Hatua
Maombi yatakayowasilishwa kwa njia ya posta, barua pepe (email) au kwa mkono hayatapokelewa.
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 04/04/2025.
2 Comments
athumanir272@gmail.com
Yani me nafaa kabisa kua askari kwa ajili ya kulinda usalama wa wanchi ukiachana na elimu yangu
Kwa nini utake watu walio soma na ambae wameishia njiani ajira Wana pata wapi au fusra kama hizi
Msibague ase wapeni watu ajira Wana weza kufanyaa m