Ifahamike kwamba, mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa muda wote wa kipindi chake Cha ujauzito.
Hatoshauriwa au kuruhusiwa kushiriki tendo la ndoa Kama ujauzito wake unachangamoto Kama vile MIMBA kutishia kutoka, anaumwa, ameshonwa mlango wa kizazi, anatokwa na damu n.k.
Mitindo ya ufanyaji tendo la ndoa wakati wa ujauzito, hubadilika kadri MIMBA inavyokuwa kubwa.
Mitindo Bora zaidi Ni ile ambayo haitochosha Wala kuleta maumivu, vyema zaidi utumike mtindo wa ubavu ubavu, mwanamke kukaa kwa juu au dog staili.
Mjamzito anapaswa kuepuka mitindo ambayo itampa maumivu ya tumbo au kumchosha zaidi. Aepuke mtindo utakao mfanya alalie mgongo kwa muda mrefu, staili ya kulalia mgongo “kifo Cha mende” kinaweza msababishia mjamzito ashindwe kupumua vizuri na kumletea shida au staili ya kulalia tumbo inaweza mkandamiza mtoto na kumsabishia matatizo.
Ikumbukwe sio kila mwanamke atakuwa na Hamu ya kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito wake hivyo asilazimishwe kufanya hivyo Kama hayuko ridhaa.
Soma hii :Njia rahisi ya Kuitambua Siku ya Kubeba mimba
Je Kufanya Tendo la Ndoa Wakati wa Ujamzito Ni Salama?
Jibu ni ndio, kufanya tendo wakati wa ujauzito ni salama kabisa. Uume kuingia ndani ya uke,zile pilika za kuingiza na kutoa haziwezi kuathiri mtoto, kwa sababu analindwa na tumbo na misuli ya ukuta wa kizazi pia.
Lakini pia mtoto analindwa na majimaji mazito(amniotic fluid).
Usijali kuhusu kusinyaa na kutanuka kwa uke pale unapofikia kilele, hakuwezi kufanya mimba ikatoka. Kutanuka huku ni tofauti na wakati wa kuzaa.
Mazingira gani inashauriwa usifanye tendo la ndoa wakati wa ujauzito?
Daktari anaweza kushauri usifanye tendo la ndoa kama
- una historia ya mimba kuharibika mara kwa mara
- uko kwenye hatari ya kupata uchungu mapema kabla ya week 37 za ujauzito
- unatokwa na damu na maumivu yasijulikana sababu yake
- chupa imepasuka na maji yanavuja
- mlango wa kizazi umefunguka mapema zaidi
- una tatizo kitaalamu placenta previa yani tishu za mirija unaomlisha mtoto chakula na hewa safi, umekuwa mpaka kuziba mlango wa kizazi
- kama unatarajia kujifungua watoto mapacha
Staili Salama za Kufanya Mapenzi Wakati wa Ujauzito
Mwanamke Ameketi :
Mwanamke anaweza kuketi juu ya mumewe, hii inamruhusu kudhibiti kina na kasi.Hii ni staili nzuri kwa sababu inampa mwanamke udhibiti zaidi juu ya kina na jinsi anavyohisi. Hii pia hupunguza shinikizo kwenye tumbo lake.
Mwanamume Ameketi
Mwanamume anaweza kuketi kwenye kiti au kitanda huku mwanamke akiwa juu yake.Katika staili hii, mwanamume anakuwa kwenye kiti au kitanda, ambayo inasaidia kuondoa uzito kutoka kwa tumbo la mwanamke.
Mwanamke Kulala Kando:
Hii ni staili salama sana kwani inasaidia kupunguza shinikizo kwenye tumbo la mwanamke na inaruhusu urahisi katika kufanya tendo.
Je naruhusiwa kupiga punyeto badala ya tendo?
Fahamu kwamba daktari akishauri usifanye tendo anamanisha pia usifanye kitu chochote ambacho kinakuamsha hisia na kukufikisha kileleni mfano kutumia dildo an vidole
Hamu ya Tendo la Ndoa wakati wa Ujauzito
Kila mwanamke mwanamke mjamzito anatofautiana namna anavojisikia kuhusu tendo. Baadhi hamu ya tendo hupotea kabisa. Wengine hufurahia zaidi tendo na kupata msisimko zaidi wa mapenzi wakati huu.
Kipindi cha ujauzito ni kawaida kwa hamu ya tendo kubadilika. Muhimu zungumza na mpenzi wako namna unavojisikia. Mueleze unapenda staili ipi nzuri ya kufanya tendo isiyokuumiza.
Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Kufanya Mapenzi
Ni muhimu kuzingatia mambo kadhaa ili kuhakikisha usalama wa mama na mtoto:
- Wasiliana na Daktari: Ni vyema kuzungumza na daktari kabla ya kuanza kufanya mapenzi ili kupata ushauri sahihi.
- Kusikiliza Mwili Wako: Ikiwa unahisi maumivu au discomfort yoyote, ni bora kusitisha shughuli hiyo.
- Kuepuka Staili Zenye Hatari: Staili ambazo zinahitaji mwanamke kulala tumboni zinapaswa kuepukwa kabisa.
Tendo la Ndoa Baada Ya Kujifungua
Kwa week 6 za mwanzo baada ya kujifungua inashauriwa usifanye tendo la ndoa. Sababu zikiwa unahitaji:-
- kupona kidonda wendapo njia ya uke ilikatwa kidogo kuongeza mlango wa mtoto kutoka
- kupona kidonda cha tumbo endapo kama ulijifungua kwa upasuaji
- uchovu kutokana na kujifungua
- mabadiliko ya homoni yatapelekea ukose hamu ya tendo kwa muda
- baaada ya kuzaa ni kawaida kuendelea kupata bleed kwa week 4 mpaka 6
- Stress kutokana na kuwaza sana kuhusu majukumu mapya kama mzazi
Kwa ujumla tendo la ndoa lifanyike baada ya mama kupona kabisa. Ongea na daktari wako akupe ushauri lini itakuwa sawa. Kwa kiasi kikubwa week 6 zinafaa kusubiri kabla ya kuanza tena tendo la ndoa. Muhimu hakikisha tu una utulivu kihisia na kimwili kabla ya kuanza .