Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, imetangaza nafasi mpya 137 za ajira katika taasisi mbalimbali za umma. Tangazo hili limetolewa rasmi tarehe 12 Juni 2025, na linahusisha ajira kutoka taasisi kama TEMESA, TANROADS, TPSC, LGTI, TICD, na TAA.
Ikiwa wewe ni Mtanzania unayetafuta kazi serikalini, fursa hii ni muhimu sana kuzingatia. Hapa chini tumekufupishia majina ya taasisi, idadi ya nafasi zilizotangazwa, pamoja na sifa za msingi.
1. Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA)
TEMESA imetangaza jumla ya nafasi 32 katika maeneo yafuatayo:
Engineer II (Marine) – 2 nafasi
Ferry Captain II – 15 nafasi
Technician II (Mechanical) – 15 nafasi
Sifa ni pamoja na Shahada au Diploma zinazotambulika katika fani husika na usajili wa kitaaluma (kwa wahandisi).
2. Tanzania National Roads Agency (TANROADS)
TANROADS imetangaza nafasi 81 katika kada mbalimbali:
Land Surveyor II – 2 nafasi
Valuer II – 2 nafasi
Weighbridge Officer II – 50 nafasi
Assistant Laboratory Technician II – 10 nafasi
Driver II – 15 nafasi
Receptionist II – 2 nafasi
Office Management Secretary II – 2 nafasi
Sifa zinatofautiana kulingana na nafasi lakini kwa ujumla ni Shahada, Diploma au Cheti na uzoefu (hasa kwa madereva).
3. Tanzania Public Service College (TPSC)
TPSC imetangaza 10 nafasi za Assistant Lecturers katika fani zifuatazo:
Mathematics/Statistics – 4 nafasi
ICT – 2 nafasi
Law – 2 nafasi
Procurement/Supplies Management – 4 nafasi
Communication Skills – 2 nafasi
Waombaji wanapaswa kuwa na Shahada ya Uzamili (GPA ≥ 3.8) na Shahada ya Awali (GPA ≥ 3.5).
4. Local Government Training Institute (LGTI)
LGTI inahitaji watumishi 3 katika nafasi zifuatazo:
Assistant Lecturer (Public Administration) – 1 nafasi
ICT Officer II (Programming) – 2 nafasi
Sifa kuu ni Shahada ya Uzamili (kwa mhadhiri) na Shahada ya kwanza (kwa ICT Officer).
5. Tengeru Institute of Community Development (TICD)
TICD imetangaza 5 nafasi za Assistant Lecturers:
Sociology – 1 nafasi
Community Development – 3 nafasi (Tangazo la Marudio)
Social Work – 1 nafasi (Tangazo la Marudio)
Sifa ni Shahada ya Uzamili GPA ≥ 3.8 na Shahada ya kwanza GPA ≥ 3.5.
6. Tanzania Airport Authority (TAA)
TAA inahitaji 2 Assistant Aircraft Marshallers. Sifa ni Cheti katika Utawala, Rasilimali Watu, Takwimu, Biashara, au fani inayofanana.