Close Menu
swahiliforums.com
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
BOFYA HAPA
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
Home » Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Zimamoto Ajira Portal)
Ajira Mpya

Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Zimamoto Ajira Portal)

Mwongozo wa Kujisajili na Kutuma Maombi Ajira za Zimamoto ,Jinsi ya Kutuma Maombi ya Ajira Kwenye Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
BurhoneyBy BurhoneyMarch 11, 2025Updated:March 11, 2025No Comments3 Mins Read
Share Facebook Twitter Telegram WhatsApp
Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Zimamoto Ajira Portal)
Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Zimamoto Ajira Portal)
Share
Facebook Twitter Telegram WhatsApp

Mfumo wa kutuma maombi ya ajira katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Tanzania Fire and Rescue Force) unafanyika kupitia mtandao rasmi wa  https://ajira.zimamoto.go.tz

Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto (Zimamoto Ajira Portal)

Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji almaharufu kama zimamoto Ajira Portal (ajira.zimamoto.go.tz) ni mfumo wa mtandao unaowezesha waombaji wa kazi katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuwasilisha maombi yao kwa njia ya kidigitali. Mfumo huu umetengenezwa kwa teknolojia ya kisasa ili kurahisisha mchakato wa ajira kwa waombaji na jeshi lenyewe.

Sifa na Vigezo vya Kujiunga

Waombaji wanapaswa kuwa na sifa zifuatazo:

  1. Raia wa Tanzania mwenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 25.
  2. Cheti cha kumaliza elimu ya sekondari (Kidato cha Nne) au shahada katika fani husika.
  3. Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au namba ya NIDA kwa ajili ya usajili.
  4. Uwezo wa kimwili na kiafya wa kutekeleza majukumu ya zimamoto na uokoaji.

Jinsi ya Kusajili Akaunti Kwenye Zimamoto Ajira Portal

Kwa waombaji wapya, hatua za awali za kujisajili ni muhimu ili kupata akaunti kwenye mfumo. Fuata hatua hizi ili kujiandikisha:

1. Tembelea Tovuti Rasmi

Fungua kivinjari (browser) chako na tembelea ajira.zimamoto.go.tz

2. Bonyeza Kitufe cha “Sign Up”

Chagua kitufe cha “Sign Up” ili kuanza mchakato wa usajili.

Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (Zimamoto Ajira Portal)

3. Weka Namba ya Utambulisho wa Taifa (NIDA)

Ingiza NIDA number yako na bonyeza Submit NIN ili kuendelea.

4. Jibu Maswali ya Uhakiki

  • Mfumo utatoa maswali ya uthibitisho wa utambulisho wako.
  • Jibu maswali mawili kwa usahihi ili kuthibitisha utambulisho wako.

5. Kamilisha Usajili

  • Mfumo utaonyesha taarifa zako zilizo kwenye rekodi ya NIDA.
  • Ingiza barua pepe yako (email), tengeneza nenosiri (password) na bonyeza Submit.

6. Thibitisha Akaunti Yako kwa Barua Pepe

Baada ya kukamilisha usajili, angalia barua pepe yako kwa ajili ya kiungo cha kuthibitisha akaunti.
Ikiwa hujaona barua pepe kwenye “Inbox”, angalia kwenye Spam Folder.

Baada ya kuthibitisha akaunti yako, sasa unaweza kuingia kwenye mfumo kwa kutumia barua pepe na nenosiri ulilounda.

Jinsi ya Kuingia Katika Akaunti

Ikiwa tayari umejisajili, fuata hatua hizi ili kuingia kwenye mfumo na kuanza kutuma maombi:

  1. Nenda kwenye ajira.zimamoto.go.tz
  2. Bonyeza kitufe cha Login
  3. Ingiza barua pepe yako na nenosiri
  4. Bonyeza Login ili kufungua akaunti yako

Jinsi ya Kuingia Katika Akaunti

Ikiwa umesahau nenosiri, bonyeza “Forgot Password”, ingiza barua pepe yako, na utapokea kiungo cha kurekebisha nenosiri kupitia barua pepe yako.

Namna ya Kujaza Taarifa kwenye Mfumo

Baada ya kuingia kwenye akaunti yako, unapaswa kujaza taarifa zifuatazo:

  1. Wasifu wa Kibinafsi: Jina kamili, anuani, maelezo ya mawasiliano.
  2. Taarifa za Elimu: Ingiza kiwango cha elimu na cheti husika.
  3. Uzoefu wa Kazi: Ikiwa una uzoefu wa kazi, jaza sehemu hii.
  4. Maombi ya Kazi: Chagua nafasi unayotaka na ambatanisha nyaraka zinazohitajika.

Jinsi ya Kutuma Maombi ya Ajira Kwenye Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

Baada ya kuingia kwenye akaunti yako, unaweza kuanza kutuma maombi ya kazi kwa kufuata hatua zifuatazo:

Nenda Kwenye “Find Job”

  • Upande wa juu kushoto wa ukurasa wako wa mwanzo, bonyeza Find Job.

Jinsi ya Kutuma Maombi ya Ajira Kwenye Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto

Chagua Nafasi ya Kazi Unayoitaka

  • Tafuta nafasi za kazi kulingana na sifa zako za kitaaluma.

Chagua Nafasi ya Kazi Unayoitaka

Bonyeza “Apply for Job”

  • Baada ya kuchagua kazi unayotaka, bonyeza kitufe cha Apply for Job.

Wasilisha Nyaraka Zako Muhimu

  • Pakia vyeti vya elimu na nyaraka nyingine muhimu kama zinavyohitajika.

Thibitisha na Kutuma Maombi

  • Hakikisha taarifa zako ni sahihi kabla ya kuthibitisha maombi.
  • Baada ya kutuma maombi, unaweza kuangalia hali ya maombi yako kwa kwenda kwenye “Applied Jobs” ndani ya akaunti yako.

Thibitisha na Kutuma Maombi

Jinsi ya Kuangalia Maombi Yako

Baada ya kutuma maombi, unaweza kuangalia hali ya maombi yako kwa:

Kuingia kwenye akaunti yako.

Kubonyeza Applied Jobs (Kazi Ulizoomba).

Kuangalia kama maombi yako yamepokelewa na yanashughulikiwa.

Follow on Telegram Follow on WhatsApp
Share. Facebook Twitter Email Telegram WhatsApp
Burhoney
  • Website

Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati

Related Posts

Nafasi 137 za Kazi Kutoka UTUMISHI – Taasisi Mbalimbali Juni 2025

June 13, 2025

Nafasi 83 za Kazi Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) June 2025

June 12, 2025

Nafasi za Kazi – NARCO (Kampuni ya Ranchi za Taifa) – Juni 2025

June 12, 2025

Majina ya Walioitwa kazini Ajira Portal Utumishi PSRS 2025 PDF Download

June 12, 2025

Majina Ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI na Ajira Portal 2025

June 12, 2025

Matokeo ya Usaili Ajira Portal 2025 / 2026 Utumishi wa Umma PSRS

June 12, 2025
Leave A Reply Cancel Reply

Latest Posts

Nafasi 137 za Kazi Kutoka UTUMISHI – Taasisi Mbalimbali Juni 2025

June 13, 2025

Nafasi 83 za Kazi Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) June 2025

June 12, 2025

Nafasi za Kazi – NARCO (Kampuni ya Ranchi za Taifa) – Juni 2025

June 12, 2025

Majina ya Walioitwa kazini Ajira Portal Utumishi PSRS 2025 PDF Download

June 12, 2025

Majina Ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI na Ajira Portal 2025

June 12, 2025
Load More

Subscribe to Updates

Usipitwe na Habari zetu za kila siku Kuwa wa kwanza kupata Habari zetu Kwa Kuandika Email yao Hapo chini

SwahiliForums Ni jukwaa la Habari na Makala mbalimbaali kwa Lugha kiswahili Habari za Michezo,Elimu, Biashara,Ajira Mpya na Dondoo za Afya Endelea kutufuatilia kwa kutembelea site yetu SwahiliForums.com

Karibu kwenye Swahiliforums, jukwaa lako la kipekee kwa habari, maarifa, na mijadala inayoangazia masuala ya kijamii, uchumi, na utamaduni kutoka kwa mtazamo wa Kiswahili. Hii ni blog ambayo inalenga kutoa taarifa za kina kuhusu matukio ya sasa, maisha ya kila siku, na masuala muhimu yanayoathiri jamii zetu katika eneo la Afrika Mashariki na duniani kwa ujumla.

swahiliforums.com
Facebook X (Twitter) Instagram WhatsApp Telegram Pinterest
Copyrights reserved @2025 swahiliforum.com

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.