Magonjwa ya zinaa (Sexually Transmitted Infections – STIs) ni magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana bila kinga. Magonjwa haya ni pamoja na kaswende, kisonono, chlamydia, virusi vya HPV, virusi vya herpes, hepatitis B na C, pamoja na UKIMWI (HIV/AIDS). Watu wengi huambukizwa bila kujua kwa sababu baadhi ya magonjwa haya hayaonyeshi dalili mapema.
Kupima magonjwa ya zinaa ni hatua muhimu sana ya kujikinga, kulinda afya ya wapenzi wetu na kuhakikisha tiba mapema. Katika makala hii, utajifunza njia mbalimbali za kupima magonjwa ya zinaa, wakati sahihi wa kupima, na faida za kufanya vipimo hivi mapema.
Ni Wakati Gani Unapaswa Kupima Magonjwa ya Zinaa?
Baada ya kufanya ngono bila kondomu na mpenzi mpya
Ukigundua kuwa mpenzi wako ana dalili au amethibitika kuwa na STI
Ukiwa na dalili kama maumivu wakati wa kukojoa, uchafu ukeni au uume, vidonda au vipele sehemu za siri
Kabla ya kuanza uhusiano mpya wa kimapenzi
Wakati wa ujauzito (kupima husaidia kuepuka maambukizi kwa mtoto)
Kwa walio katika hatari kubwa – mfano watoa huduma za afya au watu wenye wapenzi wengi
Njia za Kupima Magonjwa ya Zinaa
1. Kipimo cha Damu
Vipimo hivi hutumika kugundua magonjwa kama:
UKIMWI (HIV)
Kaswende (Syphilis)
Hepatitis B na C
Herpes (ikiwa ni maambukizi ya muda mrefu)
Mgonjwa huchukuliwa damu kidoleni au kwenye mshipa, na matokeo huweza kutolewa baada ya dakika chache au siku chache kutegemea na aina ya kipimo.
2. Kipimo cha Mkojo
Hutumika kugundua maambukizi ya:
Kisonono (Gonorrhea)
Chlamydia
Mgonjwa hutoa sampuli ya mkojo ambayo hupimwa maabara kutafuta vimelea vya magonjwa.
3. Kupima kwa Kupaka au Kuchukua Sampuli (Swab Test)
Sampuli ya majimaji huchukuliwa kutoka:
Sehemu za siri (uke, uume, njia ya haja kubwa)
Koo (kama ngono ya mdomo ilifanyika)
Swab hupelekwa maabara kuchunguza vimelea vya magonjwa mbalimbali.
4. Kipimo cha Kupima Haraka (Rapid Tests)
Vipimo hivi hutolewa katika baadhi ya vituo vya afya na kutoa matokeo ndani ya dakika 15 hadi 30. Hutumika sana kwa:
HIV
Kaswende
Hepatitis
5. Kipimo cha DNA au PCR (Polymerase Chain Reaction)
Ni kipimo cha kisasa kinachotambua vimelea vya magonjwa kwa ufanisi wa hali ya juu. Hutumika kupima:
HPV
Chlamydia
Kisonono
Faida za Kupima Magonjwa ya Zinaa
Kugundua maambukizi mapema na kupata matibabu
Kuzuia kusambaza maambukizi kwa wengine
Kuokoa maisha yako na ya mtoto kama una mimba
Kujenga mahusiano ya kuaminiana na mpenzi wako
Kuepuka madhara ya muda mrefu kama utasa au saratani ya shingo ya kizazi
Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kupima
Epuka kukojoa saa 1 hadi 2 kabla ya kipimo cha mkojo
Toa historia kamili ya mahusiano yako kwa mtaalamu
Hakikisha unapata ushauri wa kitaalamu baada ya matokeo
Usifanye ngono mpaka upate majibu sahihi
Je, Vipimo vya Magonjwa ya Zinaa Vinapatikana Wapi?
Hospitali za Serikali na Binafsi
Vituo vya afya vya ngazi ya jamii
Kliniki za afya ya uzazi
Vituo vya ushauri nasaha na upimaji wa HIV (VCT)
Maabara binafsi
Baadhi ya maduka ya dawa makubwa (vipimo vya haraka vya nyumbani)c
Je, Vipimo vya Magonjwa ya Zinaa Vinagharimu Kiasi Gani?
Gharama hutofautiana kulingana na:
Aina ya kipimo
Kituo cha afya
Umbali wa maabara
Vipimo vya msingi kama HIV, kaswende, na kisonono vinaweza kuwa bure katika hospitali za serikali. Vipimo vya kisasa kama PCR vinaweza kugharimu kuanzia TSh 20,000 hadi 100,000 au zaidi.