Nywele ndefu, zenye afya na nguvu ni ndoto ya wengi. Mojawapo ya siri za urembo wa asili kutoka kwa tamaduni za Kiasia ni matumizi ya maji ya mchele kwa nywele. Maji ya mchele yana virutubisho vinavyosaidia kukuza nywele, kuimarisha urefu wake, na kuifanya iwe yenye afya.
Faida za Maji ya Mchele kwa Nywele
- Huchochea Ukuaji wa Nywele – Maji ya mchele yana amino acids na vitamini B ambayo husaidia kuimarisha mizizi ya nywele na kukuza nywele haraka.
- Huimarisha Nywele – Yana wanga (starch) inayosaidia kuimarisha nywele dhaifu na kuzuia kukatika.
- Huongeza Mng’ao wa Nywele – Husaidia kufanya nywele kung’aa na kuwa laini kwa sababu ya protini asilia zinazopatikana ndani yake.
- Huzuia Kupasuka kwa Nywele – Virutubisho vilivyomo ndani ya maji ya mchele husaidia kupunguza matatizo ya nywele kukatika na kupasuka.
- Huimarisha Afya ya Ngozi ya Kichwa – Hupambana na mba na kuimarisha mazingira ya ngozi ya kichwa, kusaidia ukuaji mzuri wa nywele.
Jinsi ya Kutengeneza na Kutumia Maji ya Mchele kwa Nywele
1. Kutengeneza Maji ya Mchele
Malighafi:
- Vikombe 1-2 vya mchele (aina yoyote)
- Vikombe 2-3 vya maji safi
JINSI YA KUAANDA MAJI YA MCHELE
Sasa hapa mrembo wangu wacha nikudadavulie kinaga ubaga mwanzo mpaka mwishoo maana hapo juu nilirashia mambo haya hapa
- Andaa mchele wako robo kilo mchele aina yoyote ile usiwe tuu ule wa birian maana hamchelewi.
- osha vizuri kisha weka kwenye sufuria
- weka maji mengi kadri utakavyo kwenye mchele wako
- Acha ya uchemke dakika10 kwa moto wa wa stani mpaka uone mchele unaanza kulainika
- Chuja maji yako na weka kwenye kopo maji unayo ya chuja na ufunike vizuri usiku mzima, asubuhi ongeza maji kikombe kimoja ili kupunguza nguvu.
- Hifadhi maji yako kwenye friji kwa muda wa wiki mbili ya sipoteze ubora wake.
NAMNA YA KUTUMIA MAJI YA MCHELE
- Osha nywele zako kwa shampoo kama kawaida hakikisha unasugua kichwa kizima mpaka nywele zitakate
- Fanya deep conditioning kwa dakika30
- Osha tena nywele zako na maji ya kawaida
- Kisha anzakupaka yale maji ya mchele kwenye nywele hakikisha yanasamba kichwa kizima hadi kwenye ngozi, na utulie ndani ya dakika3 mpka5 kisha ndio unoshe tena na ukimaliza zikaushe nywele zako lazima utaona utofauti tuu
Najua kama ni kaprocess kidogo lakini siku zote mtaka lake hashindwi, kwanini kila siku wewe uwe unauliza wenzio unapaka dawa gani, unatumia mafuta gani kwanini usifanye ulichoelekezwa nawewe ukaona maajabu kuwa mwalimu kwa wengine, changamka sasa na ujue tuu maji ya mchele yanavitamins A,B,E na amino acid ambapo vitamin vyote hivyo vinafaida sana katika nywele zako.
Mambo Muhimu ya Kuzingatia
- Unaweza kuongeza matunda ya machungwa au mafuta ya lavender kwenye maji ya mchele ili kupunguza harufu yake.
- Ikiwa unapata ukavu mwingi wa nywele, punguza matumizi yake hadi mara moja kwa wiki.
- Kwa matokeo mazuri, hakikisha unafuata utaratibu huu mara kwa mara.