JIUNGE NASI WHATSAPP
BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM
BOFYA HAPA
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA)Wametanabaisha Gharama za usajili wa Kampuni Brela Gharama ambazo huweza kutofautiana kulingana na Ukubwa wa kampni.
Gharama za Usajili wa Kampuni
Ada ya Usajili:
- Ada za usajili wa kampuni zinaanzia Tsh 20,000 hadi Tsh 50,000,000 kulingana na mtaji wa kampuni husika. Kampuni ndogo yenye mtaji mdogo inaweza kulipa ada ya chini zaidi, wakati kampuni kubwa yenye mtaji mkubwa italipa ada zaidi.
Ada za Kampuni za Kigeni:
- Kwa kampuni za kigeni, ada ya usajili ni USD 1,190. Pia, kuna ada ya kufungua nyaraka (filing fee) ya Tsh 66,000 na ada ya stamp duty ya Tsh 6,200.
Ada za Huduma Nyingine:
- Ada ya maombi ya kusajili notisi ya kusitisha biashara ni Tsh 10,000.
- Ada ya maombi ya kusajili mabadiliko ya taarifa yoyote iliyosajiliwa ni Tsh 15,000.
- Ada ya kukagua rejesta ni Tsh 2,000.
- Nakala isiyo na ithibati ya waraka wowote chini ya uangalizi wa Ofisi ya Msajili, kwa ukurasa au sehemu ya ukurasa ni Tsh 3,000.
Gharama hizi zinajumuisha ada za msingi za usajili na zinaweza kuongezeka kulingana na huduma za ziada kama vile ushauri wa kisheria au huduma za wakala.
Soma Hii :Orodha ya Biashara Zinazoweza kukuingizia Faida ya elfu kumi kwa siku
Ada za Kampuni
1. Kampuni ambayo thamani ya hisa zake halisi ni: |
– Zaidi ya Tsh.. 20,000/= lakini si zaidi ya Tsh.. 1,000,000/= Tsh. 95,000 /= |
– Zaidi ya Tsh.. 1,000,000/= lakini si zaidi ya Tsh.. 5,000,000/= Tsh. 175,000 /= |
– Zaidi ya Tsh..5,000,000/= lakini si zaidi ya Tsh..20,000,000/= Tsh. 260,000 /= |
– Zaidi ya Tsh.. 20,000,000/= lakini si zaidi ya Tsh.. 50,000,000/= Tsh. 290,000 /= |
– Zaidi ya Tsh..50,000,000/= Tsh. 440,000 /= |
2. Usajili wa kampuni ambayo haina mtaji wa hisa ambapo idadi ya washirika ni kama ilivyoelezwa katika Malengo na Katiba ya Kampuni: Tsh. 300,000 /= |
3. Ada ya kufungua jalada kwa ajili ya maombi, maana yake Tsh.. 22,000/= kwa kila waraka, yaani Malengo na Katiba ya Kampuni. Tsh. 66,000 /= |
4. Gharama ya kila Ushuru wa stempu katika kila nakala ya Malengo na Katiba ya Kampuni ni Tsh. 10,000 /= |
5. Gharama za ushuru wa stempu katika Fomu na. 14b Tsh. 1,200 /= |
6. Kulinda jina la kampuni ni Tsh. 50,000 /= |
7. Kubadilisha jina la kampuni Tsh. 22,000 /= |
8. Gharma za upokeaji na/au usajili wa waraka wowote kwa Msajili chini ya Sheria ni Tsh. 22,000 /= |
9. Gharama za kuchelewa kufungua faili/usajili wa waraka wowote zinalipwa kwa Msajili (kwa mwezi au sehemu ya siku za mwezi) TSHS 2,500 /= |
10. Gharama za kujaza taarifa ya mwaka Tsh. 22,000 /= |
11. Gharama za ithibati ya waraka wowote kwa ukurasa ni Tsh. 3,000 /= |
12. Gharama za kutafuta jalada lolote/au kupekua kitu chochote ni Tsh. 3,000 /= |
13. Gharama kwa ajili ya ripoti ya utafutaji kwa faili ni Tsh. 22,000 /= |
14. Ada zinazolipwa na kampuni ambapo Kifungu XII cha Sheria kinahusika |
– Gharama za usajili wa nakala yenye ithibati ya mkataba, sheria au malengo na katiba ya kampuni, au muongozo mwingine au kufafanua katiba ya kampuni ni Dola za Kimarekani 750 /= |
– Gharama za ujazaji wa waraka wowote unaohitajika kupelekwa kwa Msajili chini ya Kifungu XII cha Sheria hii/mbali na mizania ni Dola za Kimarekani 220 /= |
– Gharama kwa ajili ya kufungua jalada la mizania Dola za Kimarekani 220 /= |
– Ada ya kuchelewa kufungua jalada/usajili wa waraka wowote inalipwa kwa Msajili (kwa mwezi au sehemu ya siku za mwezi) ni Dola za Kimarekani 25 /= |
15. Gharama ya kupata nakala ya Cheti cha Usajili Tsh. 4,000 /= |
.
JIUNGE NASI WHATSAPP
BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM
BOFYA HAPA