Harufu mbaya ukeni ni tatizo linalowakumba wanawake wengi, ingawa wengi wao husita kulizungumzia. Harufu hii inaweza kuathiri hali ya kujiamini, mahusiano ya kimapenzi, na hata afya kwa ujumla. Kwa bahati nzuri, kuna dawa mbalimbali – za asili na za hospitali – ambazo zinaweza kusaidia kuondoa tatizo hili kabisa.
Sababu za Harufu Mbaya Ukeni
Maambukizi ya Bakteria (Bacterial Vaginosis)
– Hii ni sababu kubwa inayosababisha harufu ya shombo ya samaki.Maambukizi ya Fangasi (Yeast Infection)
– Ingawa hayatoi harufu kali, yanaweza kuchangia mabadiliko ya harufu ya uke.Kutozingatia usafi wa sehemu za siri
– Kutotumia maji safi na kutoosha uke kwa njia sahihi hupelekea kusanyiko la bakteria.Nguo za ndani zisizo safi au zinazobana
– Huweza kushikilia jasho na kusababisha uotaji wa bakteria.Mabadiliko ya homoni
– Kipindi cha hedhi, ujauzito au menopause huathiri ute na harufu ya uke.Kuingiza vitu visivyofaa ukeni (mf. sabuni kali, scented sprays, douches)
– Hupunguza kinga ya asili ya uke na kuleta maambukizi.Magonjwa ya zinaa (STIs)
– Kama Trichomoniasis huambatana na harufu mbaya kali.
Dalili Zinazoambatana na Harufu Mbaya
Kutokwa na uchafu wenye rangi ya kijivu au njano
Muwasho na kuwashwa ukeni
Maumivu wakati wa kukojoa au kujamiiana
Kuvimba kwa midomo ya uke (vulva)
Kutokwa na damu isiyo ya kawaida kati ya hedhi
Dawa za Kuondoa Harufu Mbaya Ukeni
1. Dawa za Asili
a. Maji ya Mwarobaini
Chukua majani mabichi ya mwarobaini, chemsha kwa dakika 10.
Acha yapoe, kisha tumia maji hayo kunawa sehemu za siri mara 2 kwa siku.
b. Karafuu
Chemsha karafuu 5-10 kwenye maji.
Tumia maji haya baada ya kupoa kuosha uke kwa siku 3 hadi 5.
c. Majani ya Mpera
Chemsha majani ya mpera, subiri yapoe.
Tumia maji hayo kusafisha sehemu za siri, husaidia kuondoa harufu na kuua bakteria.
d. Unga wa manjano + asali
Manjano ina antibacterial, asali huzuia fangasi.
Changanya na maji kidogo, paka kwa dakika 10, suuza mara 2 kwa wiki.
e. Uji wa mtama au togwa ya uwele
Husaidia kurekebisha bakteria wazuri tumboni na mwilini, na hivyo kusaidia usawa wa uke.
2. Dawa za Hospitali
Ikiwa harufu mbaya imesababishwa na maambukizi, daktari anaweza kuagiza:
Metronidazole (Flagyl) – dawa ya vidonge au cream kwa bakteria
Clindamycin cream – hutumika ukeni kwa maambukizi ya bakteria
Fluconazole – kwa maambukizi ya fangasi
Antibiotics nyingine – kwa magonjwa ya zinaa (STIs)
Muhimu: Usitumie dawa bila vipimo na ushauri wa daktari. Kila maambukizi hutibiwa kwa dawa tofauti.
Njia za Kuzuia Harufu Mbaya Ukeni
Osha uke kwa maji safi na vuguvugu pekee – epuka sabuni zenye manukato.
Badilisha chupi angalau mara 2 kwa siku – tumia za pamba.
Epuka kuvaa nguo za kubana muda mrefu.
Jisaidie haja ndogo kabla na baada ya tendo la ndoa.
Epuka “douching” – kuingiza maji au sabuni ndani ya uke.
Tumia pedi safi na ubadilishwe mara kwa mara wakati wa hedhi.
Kunywa maji mengi kila siku.
Kula matunda yenye probiotics kama mtindi wa kawaida (yogurt).
Maswali na Majibu (FAQs)
Je, ni kawaida uke kuwa na harufu?
Ndiyo. Uke una harufu yake ya asili, lakini harufu ya shombo ya samaki au kali si ya kawaida.
Je, sabuni ya kawaida inaweza kuondoa harufu?
Hapana. Sabuni nyingi huua bakteria wazuri wa uke na kuongeza tatizo. Tumia maji pekee au dawa asili.
Harufu mbaya huisha yenyewe?
Si mara zote. Ikiwa ni kwa sababu ya maambukizi, huhitaji tiba ya kitaalamu.
Nitajuaje kama nina maambukizi?
Dalili ni pamoja na harufu kali, kutokwa na uchafu wa ajabu, muwasho au maumivu wakati wa kukojoa.
Je, unaweza kupata harufu mbaya hata ukiwa msafi?
Ndiyo. Sababu zinaweza kuwa maambukizi, homoni au vyakula fulani unavyokula.