Close Menu
swahiliforums.com
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
BOFYA HAPA
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
Home » Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Uchungu kwa Mjamzito.
Afya

Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Uchungu kwa Mjamzito.

BurhoneyBy BurhoneyMarch 14, 2025Updated:March 14, 2025No Comments4 Mins Read
Share Facebook Twitter Telegram WhatsApp
Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Uchungu kwa Mjamzito.
Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Uchungu kwa Mjamzito.
Share
Facebook Twitter Telegram WhatsApp
WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Uchungu wa uzazi ni hatua ya kwanza ya kujifungua. Wakati wa uchungu wa uzazi misuli ya tumbo lako la uzazi (uterasi) inabana tena na tena ili kumsukuma mtoto wako nje. Mikazo hii huitwa uchungu wa kuzaa. Mikazo huacha na kuanza yenyewe. Huna udhibiti wowote juu yenyewe.

Zifuatazo ni Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Dalili za Mwanzoni za Uchungu.

1. Maumivu ya Mgongo na Kiuno Wakati fulani.
Wajawazito wengi hupata Maumivu haya kutokana na Ongezeko la Homoni ya Relaxin ambayo hulegeza Nyonga kwa ajili ya kuhakikisha kuwa Mtoto anaweza kupita kwenye Nyonga, wakati Mwingine hii Homoni huweza kuathiri Jointi na Ligamenti za Mwili mzima na Mjamzito hupata Maumivu Jointi nyingine za Mwili wake.

2. Mtoto Kushuka (Lightening).
Kuanzia Wiki ya 32 Mara nyingi Mtoto hushuka kwenda kwenye Nyonga tayari kwa ajili ya Kuzaliwa na Kutoka Duniani.

3. Kukojoa Mara kwa Mara.
Baada ya Mtoto Kushuka Mjamzito huanza kupata Dalili za Kukojoa Mara kwa Mara, Ni kwa sababu Kibofu Cha Mkojo hugandamizwa na sehemu ya Mtoto ambayo iko Chini kwenye Nyonga ya Mjamzito na kubanwa kwa Kibofu Kati ya sehemu hiyo ya Mtoto na Mfupa wa Kinena.

4. Kuchoka Mara kwa Mara na Kukosa Usingizi.
Maumivu katika kipindi cha Mwishoni mwa Ujauzito na Kukojoa Mara kwa Mara hii hupelekea Mjamzito kukosa Usingizi wa kutosha hivyo Muda mwingi huwa na Uchovu wa Mara kwa Mara.

5. Uzito kutoongezeka.
Kwa kawaida Mjamzito huongezeka Uzito wa Wastani wa 1kg katika kila Mwezi mmoja katika Kipindi cha Ujauzito lakini inapofika Mwishoni mwa Ujauzito Uzito huwa hauongezeki na wakati mwingine inawezekana kabisa Uzito hupungua ndio maana ni vema inapofikisha Wiki 42 ujifungue na hutakiwi kuzidisha Wiki 43 za Ujauzito.

SOMA HII :  Kiwango sahihi cha sukari mwilini

6. Kuharisha.
Baadhi ya Wajawazito hupata Dalili ya Kuharisha hii ni Kutokana na Ongezeko la Homoni za Prostaglandins ambazo hupelekea Mfuko wa Uzazi kujikunja na kuweza kutoa Mtoto Wakati wa Kujifungua lakini pia huweza kupelekea Ongezeko kubwa la mjongeo wa Utumbo Mdogo hivyo huweza kupelekea Dalili za Kuharisha kwa Mjamzito.
Hutofautiana kati ya Mjamzito moja na mwingine.

7. Maumivu ya Kubana na Kuachia.
Maumivu ya kubana na kuachia hutokea katika kipindi chote Cha Ujauzito, Lakini endapo Maumivu hayo hayana Mpangilio maalumu basi huwa ni Dalili za Mwanzoni za Kujifungua tofauti na Uchungu Kamili ambapo Maumivu huongezeka kadiri Muda unavyoenda na huwa na Mpangilio maalumu.

8. Mtoto kupunguza kucheza.
Kwa kawaida Wajawazito huanza kuhisi Mtoto kucheza kuanzia Wiki ya 20 kwenda juu na Mtoto huongezeka kucheza kadiri umri wa Mimba unavyoongezeka na kufikia Wiki ya 32 Mtoto hucheza zaidi baada ya hapo Mtoto hupunguza Kucheza kwa sababu anakuwa ameshuka kwenye Nyonga tayari kwa ajili ya Kutoka na Kuzaliwa.

Soma hii :Faida Za Kufanya Mapenzi Wakati wa Ujauzito

Ni nini hufanyika wakati wa uchungu wa uzazi?

Mlango wako wa kizazi ni sehemu ya chini ya uterasi yako ambapo inaunganishwa na uke wako. Mlango wa kizazi una mwanya mdogo ambao hubaki ukiwa umefungwa kabisa unapokuwa mjamzito. Wakati wa uchungu wa uzazi, mikazo yako polepole huvuta mlango wa kizazi na kuufungua hadi upanuke vya kutosha kwa mtoto wako kutoka.

Uchungu wa uzazi una sehemu 2:

  • Uchungu wa uzazi wa mapema

  • Uchungu wa uzazi unaoendelea

Wakati wa uchungu wa uzazi wa mapema:

  • Shingi yako ya kizazi huanza kuwa nyembamba na kufunguka takriban inchi 1 hadi 2 (sentimita 2 hadi 5)

  • Mikazo huja na kuondoka na kupata nguvu na kugawanyika kwa usawa zaidi

  • Maumivu haya siyo mabaya sana

SOMA HII :  Dalili za mtu mwenye msongo wa mawazo

Wakati wa uchungu wa uzazi unaoendelea:

  • Mlango wako wa kizazi hufunguka kikamilifu, takriban inchi 4 (sentimita 10) na kubana kabisa.

  • Mtoto wako anashuka (husogea chini kwenye fupanyonga lako na kuwa tayari kuingia kwenye njia ya uzazi)

  • Unaanza kujisikia kama unahitaji kusukuma mtoto nje

  • Maumivu ni makali zaidi

kupasuka kwa chupa yako ya uzazi ni wakati mfuko wa amnioti hupasuka na kiowevu cha amnioti kutoka kwenye uke wako. Hii inaweza kutokea kabla ya kuanza kwa uchungu wa uzazi au wakati wa uchungu wa uzazi.

Follow on Telegram Follow on WhatsApp
Share. Facebook Twitter Email Telegram WhatsApp
Burhoney
  • Website

Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati

WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Related Posts

Jinsi ya kuacha kujichua kwa mwanamke

December 2, 2025

Kazi ya vipipi ukeni

December 2, 2025

Jinsi ya kutumia vipipi mahaba

December 2, 2025

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume

December 2, 2025

Tabia ya mtoto wa kiume akiwa tumboni

December 2, 2025

Jinsi ya kutumia pipi kifua kwa mwanamke

December 2, 2025

Comments are closed.

Latest Posts

Zimamoto Recruitment Portal Login:Mfumo wa Maombi ya Ajira Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

December 13, 2025

Majina ya Walioitwa kwenye Usaili Jeshi la Zima moto PDF Download December 2025

December 12, 2025

MAJINA Walioitwa Kwenye Usaili MDAs & LGAs 2026

December 12, 2025

Orodha ya Majina walioitwa kwenye Usaili kada ya Afya na Ualimu Ajira portal December 2025

December 4, 2025

Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Kada za Afya na Elimu TAMISEMI

November 26, 2025
Load More

Subscribe to Updates

Usipitwe na Habari zetu za kila siku Kuwa wa kwanza kupata Habari zetu Kwa Kuandika Email yao Hapo chini

SwahiliForums Ni jukwaa la Habari na Makala mbalimbaali kwa Lugha kiswahili Habari za Michezo,Elimu, Biashara,Ajira Mpya na Dondoo za Afya Endelea kutufuatilia kwa kutembelea site yetu SwahiliForums.com

Karibu kwenye Swahiliforums, jukwaa lako la kipekee kwa habari, maarifa, na mijadala inayoangazia masuala ya kijamii, uchumi, na utamaduni kutoka kwa mtazamo wa Kiswahili. Hii ni blog ambayo inalenga kutoa taarifa za kina kuhusu matukio ya sasa, maisha ya kila siku, na masuala muhimu yanayoathiri jamii zetu katika eneo la Afrika Mashariki na duniani kwa ujumla.

swahiliforums.com
Facebook X (Twitter) Instagram WhatsApp Telegram Pinterest
Copyrights reserved @2025 swahiliforum.com

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.