Close Menu
swahiliforums.com
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
BOFYA HAPA
  • Home
  • Ajira Mpya
  • Elimu
  • Michezo
  • Makala
Facebook X (Twitter) Instagram
swahiliforums.com
Home » Dalili za Hatari Kwa Mjamzito Zinazopelekea Mimba Kuharibika
Afya

Dalili za Hatari Kwa Mjamzito Zinazopelekea Mimba Kuharibika

Dalili 6 Hatari Kwa Mjamzito Zinazopelekea Mimba Kuharibika
BurhoneyBy BurhoneyMarch 28, 2025Updated:March 28, 2025No Comments3 Mins Read
Share Facebook Twitter Telegram WhatsApp
Share
Facebook Twitter Telegram WhatsApp
WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Kwa mama Mjamzito Hasa wenye Mimba changa kuna Dalili au ishara Ukiziona wakati wa mimba yako hasa ikiwa changa jua ni hatari zinaweza kuashiria Mimba yako inaharibika au kutoka hivyo Ukiona Dalili Moja ama zote kati ya zifuatazo muone Daktari.

Dalili za Kawaida Ambazo siyo hatarishi

Dalili nyingi kati ya hizi siyo hatari, na haitakiwi kupata hofu sana. Japo unaruhusiwa kumpigia daktari wako na kumuuliza ili upate uhakika zaidi. Dalili nyingi ya hizi zinajitokeza mimba ikiwa changa, na zingine baadae

  • kutapika
  • kutokwa na uchafu mwingi ukeni
  • kichwa kuuma
  • uchofu na kizunguzungu
  • maumivu yanayokuja kwa haraka na kupotea
  • kupungua uzito
  • kuhisi joto kali
  • kushindwa kuvuta hewa vizuri
  • mawazo, na kupata hofu ana kushindwa kufanya kazi zako vizuri

Dalili hizi zinatokea mda wowote wa ujauzito. Japo mimba inapokuwa changa zaidi ndipo hatari ya mimba kuharibika inakuwa kubwa, ila watakiwa kuwa makini kipindi chote.

1. DAMU UKENI
hata kama utaona spotting/vitone vidogo vya damu usikubali mtu akwambie ni kawaida jinyanye nenda hospital mapema ukafanyiwe vipimo

2. KUVIMBA MWILI MZIMA
hii mara nyingi husababishwa na presha kuwa juu mama anaweza kuvimba miguu sana na uso na mikono pia. Ukiona hii dalili wahi hospital

3.MAUMIVU YA TUMBO
Kuna yale maumivu ya kawaida yanayosababishwa na uterus kutanuka hasa kuanzia 2nd trimester haya hayana shida ila kuna maumivu makali sana ambayo hayavumiliki, ukipata hayo wahi mapema

4. KUACHA KUONA, KICHWA KUUMA KULIKO KAWAIDA
Hizi zinaweza kuwa dalili za presha na sukari ya mwili kutokuwa sawa ni muhimu kuhakikisha unafika hospital kupata msaada

5. HOMA KALI NA DEGEDEGE

SOMA HII :  Dawa ya asili ya uchafu mweupe ukeni

6. CHUPA KUPASUKA KABLA YA UCHUNGU
Hata kama imefika week zako za kujifungua ukiona chupa imepasuka maji yanatoka ukeni kwa mfululizo na huna dalili za uchungu wahi mapema hospital usianze kusubiri uchungu uanze

7. MAJI KUTOKA UKENI
Wapo ambao hupata hii hali mapema njia inaweza kuwa inafunguka kutokana na kazi nzito hivyo mama anapata leakage maji kutoka kidogo kidogo ni vyema kwenda ufanyiwe uchunguzi isijepelekea maji yakapungua au kuisha kwa mtoto na wakati muda wa kuzaliwa bado.

8.Kutapika na kichefuchefu kupita kiasi

Kwa mjamzito ni kawaida kupata kichefuchefu, lakini kama tatizo ni kubwa inaweza kuashiria shida kubwa ya kiafya. Kama unashindwa mpaka kula au kunywa chochote, hapo utaishiwa maji. Na kuishiwa maji inaweza kuhatarisha ujauzito wako.

Kama unahisi kizunguzungu kinakutesa sana, ongea na daktari atakupa dawa ya kupunguza makali yake.

9.Mtoto kuacha kucheza

Mtoto kupunguza kucheza inaweza kuashiria kachoka, hii ni kawaida isikupe hofu. ila kama hachezi kabisa kwa siku nzima, hapo kuna shida kubwa.

Sasa ili kugundua tatizo, inashauriwa ukiona mtoto hachezi mda mefu, jaribu unywe kitu cha baridi. Kisha lala kwa ubavu, na fatilia kama mtoto ataanza kucheza.

Mpigie daktari, ama nenda hospital haraka endapo utagundua mtoto ameacha kucheza. Daktari atafanya vipimo kuona kama kuna hatari yoyote.

10.Kupata uchungu mapema mimba ya miezi 7

Kupata uchungu na mimba haijatimiza umri wa kujifungua, ni dalili mbaya. Kama tumbo linavuta na kuachia na hii hali itokee mara chache na kuisha hilo ni kawaida. Kwani hata ukifika kileleni baada ya tendo, lazima utahisi tumbo kuvuta.

11.Chupa kupasuka mapema ni dalili mbaya kwa mjamzito

SOMA HII :  Dawa ya asili ya kuondoa chunusi na madoa usoni

Tunaposema chupa, tunamaanisha ule mfuko unaobeba mtoto. Mfuko huu unakuwa na maji yanayomlinda mtoto asiumie. Mfuko unapasuka pale mama akianza uchungu na yupo tayari kujifungua. Endapo mfuko utapasuka mapema na mtoto akaendelea kubaki tumboni, mtoto atakosa hewa na kupoteza uhai.

12.Maumivu makali yasiyoisha kwenye kichwa, tumbo na kushindwa kuona vizuri

Hizi dalili zinaweza kuashiri kupanda kwa presha kitaalamu (preeclampsia) . Hili ni tatizo baya na linaweza kupelekea kifafa cha mimba. Tatizo linaambatana na dalili za presha kupanda na protini nyingi kwenye mkojo, hasa inatokea baada ya week 20 za ujauzito. Hakikisha unaenda hospital haraka endapo unahisi dalili hizo.

Follow on Telegram Follow on WhatsApp
Share. Facebook Twitter Email Telegram WhatsApp
Burhoney
  • Website

Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati

WhatsApp Group Join Now
Telegram Group Join Now

Related Posts

Je Fistula inatibika?

October 27, 2025

Aina za fistula

October 27, 2025

Ugonjwa wa fistula kwa wanaume

October 27, 2025

Dalili za ugonjwa wa Fistula, Sababu na Tiba

October 27, 2025

Jinsi ya kuandaa unga wa mbegu za parachichi

September 14, 2025

Mafuta ya Mbegu za Maboga

September 14, 2025

Comments are closed.

Latest Posts

Majina ya Walioitwa Kwenye Mafunzo Kusimamia Uchaguzi October 2025 :INEC Tume ya Taifa ya Uchaguzi

October 19, 2025

Majina ya Walioitwa kwenye Usaili kusimamia uchaguzi 2025 – INEC Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi

October 12, 2025

Nafasi 70 Za Kazi Unitrans Tanzania Limited Madereva wa Malori 2025

September 17, 2025

Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Halmashauri ya Wilaya ya Karatu 2025

September 13, 2025

Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo 2025

September 13, 2025
Load More

Subscribe to Updates

Usipitwe na Habari zetu za kila siku Kuwa wa kwanza kupata Habari zetu Kwa Kuandika Email yao Hapo chini

SwahiliForums Ni jukwaa la Habari na Makala mbalimbaali kwa Lugha kiswahili Habari za Michezo,Elimu, Biashara,Ajira Mpya na Dondoo za Afya Endelea kutufuatilia kwa kutembelea site yetu SwahiliForums.com

Karibu kwenye Swahiliforums, jukwaa lako la kipekee kwa habari, maarifa, na mijadala inayoangazia masuala ya kijamii, uchumi, na utamaduni kutoka kwa mtazamo wa Kiswahili. Hii ni blog ambayo inalenga kutoa taarifa za kina kuhusu matukio ya sasa, maisha ya kila siku, na masuala muhimu yanayoathiri jamii zetu katika eneo la Afrika Mashariki na duniani kwa ujumla.

swahiliforums.com
Facebook X (Twitter) Instagram WhatsApp Telegram Pinterest
Copyrights reserved @2025 swahiliforum.com

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.