Mara nyingi wanaume hudhani wao ndio huwa na jukumu la kuanzisha mazungumzo ya kimapenzi, lakini ukweli ni kwamba wanawake pia huonyesha dalili za kutongoza – japo kwa njia za kisiri na zenye akili nyingi. Wanawake wanaweza kutumia ishara ndogo au mienendo fulani kumvutia mwanaume na kuonyesha kuwa wanavutiwa naye.
1. Kumtazama Mwanaume Mara Kwa Mara
Mwanamke anaweza kumtazama mwanaume mara kwa mara, hasa bila sababu ya moja kwa moja. Macho yake huonyesha kuwa anataka aonekane au kuanzisha connection ya kimapenzi.
2. Kutabasamu Mara Kwa Mara Anapokuwa Karibu Nawe
Tabasamu ni silaha ya mwanzo kabisa ya kutongoza. Mwanamke atajitahidi kutabasamu kila mara ukiwa karibu, hata kama hamna jambo kubwa mlilozungumza.
3. Kujifanya Anauliza Maswali Madogo Madogo
Anaweza kukuuliza vitu ambavyo angeweza kujua bila msaada wako, kama vile “Umevaa perfume gani?” au “Hii ni chai ya aina gani?” – lengo ni kuanzisha mazungumzo.
4. Kuwa Karibu Nawe Kwa Bahati Mbaya-Bahati Mbaya
Anakaa karibu nawe kwenye vikao, kwenye daladala, kazini au hata anapanga kuwa sehemu unayokuwepo. Hii ni njia ya kukuonyesha yuko comfortable na uwepo wako.
5. Kumgusa Mwanaume “Kibahati Mbaya”
Anaweza kugusa bega lako, mkono wako au hata kukugusa kidogo kwa kisingizio cha ucheshi au salamu – ishara ya kujenga ukaribu wa kimwili.
6. Kumupongeza Kwa Sauti Ya Upole
Mwanamke anapomwambia mwanaume, “Umevaa vizuri leo”, “Sauti yako ni nzuri sana”, au “Unajua una akili sana” kwa sauti ya chini na yenye mvuto, anakuwa anamvutia kwa makusudi.
7. Kumpa Mwanaume Kipaumbele
Anajali unachopenda, anakutumia meseji kabla hujatuma, au anahakikisha amekujibu haraka kuliko wengine.
8. Kucheka Kila Ukitupa Ucheshi
Anaweza kucheka hata kama ucheshi wako si mkubwa sana, kwa sababu anataka kukuonyesha kuwa anaenjoy company yako.
9. Kutumia Lugha Ya Mwili Ya Kuvutia
Anasimama au kukaa kwa mkao unaovutia. Anaangalia macho yako, anavua nywele usoni au anaonyesha shingo yake – yote haya ni lugha ya mwili ya kutongoza.
10. Kuposti Mitandaoni Kitu Ambacho Anajua Utaona
Anaweza kuposti picha, nukuu au status ya moja kwa moja kukuvutia, akijua utaiona.
11. Kukutumia Meseji Bila Sababu Ya Moja Kwa Moja
Anakuuliza “umekula?”, “unaendeleaje?”, “leo sijakuskia kabisa” – meseji hizi mara nyingi ni mwanzo wa kujenga mvuto.
12. Kujaribu Kukuuliza Maswali Binafsi
Anauliza kuhusu maisha yako ya uhusiano, kile unachopenda kwa mwanamke au matarajio yako ya baadaye – dalili kuwa anavutiwa.
13. Kukupa Jina La Utani
Anakutengenezea jina la kipekee kama “boss”, “handsome”, “mtoto wa mama” au “my guy” – hujenga ukaribu wa kipekee.
14. Kufurahia Kila Mara Unapompongeza
Anapotabasamu sana, kushukuru kwa bashasha na kuuliza “kweli?” unapomsifia – anakuonyesha anafurahia mvuto wako.
15. Kumtumia Mwanaume Picha Zake Za Kawaida
Hii ni njia ya kuonyesha ukaribu zaidi. Anaweza kusema “hii picha niliipiga jana, unafikiriaje?” huku akitaka asifiwe au kupokea maoni yako.
16. Kukuambia Mambo Yake Ya Ndani
Anapokueleza mambo binafsi kuhusu familia, maisha au hisia zake, anataka ujue yuko comfortable kuwa karibu nawe.
17. Kumtetea Mwanaume Mbele Ya Wengine
Kama kuna mtu anakushambulia au kukukosoa, na yeye anakutetea au anaonyesha msimamo wako ni sahihi – hiyo ni ishara kubwa ya hisia.
18. Kumuulizia Kama Ana Mpenzi
Swali hili mara nyingi haliji bure. Mwanamke anapouliza kama una mpenzi, anataka kujua nafasi yako.
19. Kujifanya Ana Mvuto Kwako Kisha Kucheka
Anaweza kusema, “Unajua, najua uko na mvuto wa kipekee lakini naogopa kukuambia” – halafu acheke. Hii ni flirtation ya moja kwa moja.
20. Kumwambia Moja Kwa Moja Ana Mvuto
Hii ni nadra, lakini wanawake wengine huamua kumwambia mwanaume wazi: “Wewe ni mzuri sana kwa macho yangu.” Wanaume wachache hupata hii zawadi.