Jinsi Ya Kuteka Attention Ya Mpenzi Wako Ambaye Anakupuuza

Jinsi Ya Kuteka Attention Ya Mpenzi Wako Ambaye Anakupuuza
Jinsi Ya Kuteka Attention Ya Mpenzi Wako Ambaye Anakupuuza

Katika mahusiano ya kimapenzi, ni kawaida kupitia vipindi ambapo mmoja anahisi kupuuzwa na mpenzi wake. Huenda unamtumia ujumbe hastaki kujibu, unapiga simu hazipokelewi, au hata anakuwa na baridi ya ghafla bila maelezo. Hali hii inaweza kuvunja moyo na kukuacha ukijiuliza: “Nitafanya nini ili niweze kumrudisha kwenye hali ya awali?” Makala hii inakupa mbinu madhubuti za kuteka tena attention ya mpenzi wako bila kujidhalilisha.

Sababu Kuu Zinazofanya Mpenzi Kupuuza

Kabla hujateka tena akili yake, ni muhimu kuelewa kwa nini anakupuuza:

  • Amechoshwa na mwelekeo wa mahusiano

  • Kuna kitu kimemkwaza lakini hajakiwasilisha

  • Anahitaji “space” kwa muda

  • Anajaribu kukuonyesha kuwa kuna kitu hakipo sawa

  • Amepoteza feelings au kuna mwingine

 Jinsi ya Kuteka Attention Yake Tena Bila Kumuandama

1. Punguza mawasiliano kwa muda

Ukigundua unajitahidi sana lakini hupati majibu, punguza kabisa mawasiliano. Hii humfanya ajiulize kwa nini umenyamaza, na mara nyingi huleta curiosity.

2. Jihusishe na maisha yako binafsi

Onesha maisha yako yanaendelea. Post picha zako ukifanya shughuli mpya, ukiwa na marafiki au ukiwa bize na kazi zako. Sio show off, bali kuonyesha kuwa haujafungwa na mahusiano tu.

3. Tumia maneno yenye mvuto na ujumbe mfupi

Badala ya kumwandikia paragraph 10, tuma sentensi moja yenye hisia:

“Siku moja tukikumbushana haya, tutajicheka sana. Natamani iwe leo.”

4. Badilisha muonekano wako

Kubadilisha muonekano wako (mtindo wa nywele, mavazi, hata maneno) kunaweza kuvuta tena macho yake. Mabadiliko huamsha hisia mpya.

5. Mshirikishe kwa njia isiyo ya moja kwa moja

Post status yenye ujumbe wa maana, ambao unamgusa bila kumtaja. Mfano:

“Ukitulia sana, unaweza kusikia kilio cha moyo wako.”

6. Mpe nafasi ya kuja kwako

Wanaume/wanawake wengi hupuuza kwa sababu wanajua hautoki. Wakati mwingine kuonyesha kuwa unaweza kuendelea na maisha yako bila kulazimisha kunavuta zaidi.

SOMA HII :  Zijue Hatua Za Kumfanya Mwanamke Akutamani

Soma Hii: Siri 100 za kumfanya mpenzi wako akumiss kila muda mpaka ahisi kuchanganyikiwa

MASWALI YANAYOULIZWA MARA KWA MARA

1. Je, kupunguza mawasiliano siyo sawa na kumpoteza kabisa?

Hapana. Kupunguza mawasiliano kunampa nafasi ya kukutamani tena. Ukijiweka sana, anaweza kukuona wa kawaida sana.

2. Nifanye nini kama ananipuuza lakini bado naonyesha kunijali kwa mbali?

Muwekee mipaka ya kimaelewano. Uliza kwa upole kama kuna tatizo, lakini usimsumbue kila mara. Mpe nafasi ajieleze mwenyewe.

3. Je, ni sahihi kumuonyesha najali wakati ananipuuza?

Ni sahihi kwa kiasi, lakini usionekane unamfuatafuata. Onyesha upendo kwa heshima, bila kuonekana tegemezi wa kihisia.

4. Kuna muda gani mzuri wa kujaribu kuwasiliana tena baada ya kupuuzwa?

Baada ya siku 3–5, unaweza kutuma ujumbe wa kawaida (sio wa malalamiko). Kama hajajibu, ruhusu muda zaidi au acha kabisa.

5. Iwapo najua amenipuuza kwa makusudi ili aniumize, nifanye nini?

Hapo unapaswa kutathmini upya thamani yako. Mtu anayekupuuza makusudi ili akuumize hana nafasi kwenye maisha yako ya baadaye. Heshimu hisia zako.

About Burhoney 4809 Articles
Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati