From Five Selection 2025 Dodoma – Waliochaguliwa Kidato cha Tano 2025 Dodoma

From Five Selection 2025 Dodoma – Waliochaguliwa Kidato cha Tano 2025 Dodoma
From Five Selection 2025 Dodoma – Waliochaguliwa Kidato cha Tano 2025 Dodoma

Baada ya kutangazwa kwa matokeo ya Kidato cha Nne 2024, hatua inayofuata ni mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano. Mkoani Dodoma, kama ilivyo kwa mikoa mingine ya Tanzania, wanafunzi waliofaulu hupewa nafasi katika shule mbalimbali za Advance kulingana na ufaulu wao na nafasi zilizopo.

Jinsi ya Kuangalia Selection za Form Five Mkoani Dodoma

Hatua za Kufuatilia Majina ya Waliochaguliwa:

  1. Tembelea tovuti rasmi ya TAMISEMI:
     https://selform.tamisemi.go.tz

  2. Bonyeza sehemu iliyoandikwa “Selection Kidato cha Tano 2025”

  3. Chagua Mkoa – Dodoma

  4. Teua Halmashauri inayokuhusu au utafute jina moja kwa moja kwa kutumia:

    • Jina la mwanafunzi

    • Au namba ya mtihani

  5. Tazama shule aliyopangiwa mwanafunzi na tahasusi (combination).

Angalizo: Kama jina halionekani, hakikisha unatumia taarifa sahihi. Pia, hakikisha umetembelea tovuti sahihi ya TAMISEMI.

 Halmashauri za Mkoa wa Dodoma

Mkoa wa Dodoma una halmashauri mbalimbali ambazo husimamia elimu ya sekondari na shule za Advance katika maeneo yao.

Orodha ya Halmashauri za Dodoma:

  1. Dodoma City Council

  2. Bahi District Council

  3. Chamwino District Council

  4. Chemba District Council

  5. Kondoa Town Council

  6. Kondoa District Council

  7. Kongwa District Council

  8. Mpwapwa District Council

Kila halmashauri ina shule moja au zaidi zinazotoa elimu ya sekondari ya juu (A-Level) na hushirikiana na TAMISEMI kusimamia uratibu wa wanafunzi wanaojiunga.

 Shule za Advance za Mkoa wa Dodoma

Dodoma ni miongoni mwa mikoa yenye shule nzuri za sekondari za Advance zenye kutoa tahasusi za sayansi, sanaa na biashara. Baadhi ya shule zina historia nzuri ya ufaulu mzuri kitaifa.

Mfano wa Shule Maarufu za Advance:

  • Dodoma Secondary School

  • Mlimwa Secondary School

  • Kongwa Secondary School

  • Mpwapwa Secondary School

  • Mazae Secondary School

  • Bihawana Secondary School

  • Kondoa Girls Secondary School

  • Chamwino Secondary School

SOMA HII :  Chuo cha Ualimu Dindimo Teachers College Joining Instructions Download PDF

Shule hizi huchukua wanafunzi kulingana na ufaulu wao kwenye masomo ya msingi ya tahasusi (PCM, PCB, EGM, HGL, CBG n.k.)

 Jinsi ya Kupata Form Five Joining Instruction – Dodoma

Fomu ya Joining Instruction ni nyaraka muhimu kwa mwanafunzi kabla ya kuripoti shule. Inajumuisha:

  • Mahitaji ya mwanafunzi (mavazi, vifaa, nk.)

  • Ada na michango ya shule

  • Tarehe ya kuripoti

  • Maelekezo ya nidhamu na usalama

  • Maelezo ya usafiri na mawasiliano ya shule

Namna ya Kupakua Fomu:

  1. Tembelea tovuti ya TAMISEMI:
     https://selform.tamisemi.go.tz

  2. Chagua sehemu ya “Joining Instructions”

  3. Andika jina la shule aliyopangiwa mwanafunzi au chagua kwa kutumia mkoa → halmashauri → shule

  4. Pakua fomu kwa kubonyeza “Download PDF”

Fomu hiyo inapaswa kuchapishwa na kusainiwa sehemu zinazotakiwa kabla ya mwanafunzi kuripoti.

About Burhoney 4816 Articles
Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati