Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS)

Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS)
Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS)

Catholic University of Health and Allied Sciences, maarufu CUHAS, ni moja ya vyuo vikuu vya afya vinavyoongoza nchini Tanzania. Chuo hiki kinajulikana kwa kutoa elimu ya ubora katika taaluma za afya na sayansi ya afya, na kutoa fursa za masomo hadi ngazi ya shahada ya uzamili (Masters) na utafiti (PhD).

Kuhusu Chuo – CUHAS

Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS) ni chuo kikuu cha afya cha binafsi kilichopo Mwanza, mkoa wa Mwanza, Tanzania. Chuo kiko katika eneo la Bugando Hill ndani ya Bugando Medical Centre (BMC) Premises, ambapo wanafunzi hupata mafunzo ya pamoja ya nadharia na vitendo kwa kushirikiana na hospitali ya rufaa ya Bugando Medical Centre.

 Historia Fupi

CUHAS ilianzishwa kama chuo cha afya kupata wataalamu wenye ujuzi unaohitajika kwa sekta ya afya nchini. Inajulikana kwa “Discipline, Diligence, Excellence” – Yaani nidhamu, bidii na ubora.

Kozi Zinazotolewa

CUHAS inatoa kozi mbalimbali katika ngazi tofauti za elimu ya juu, zikiwemo Diploma, Shahada, Uzamili na PhD.

 Programu za Diploma

  • Diploma katika Pharmaceutical Sciences

  • Diploma katika Medical Laboratory Sciences

  • Diploma katika Diagnostic Radiography

 Shahada za Kwanza (Bachelor / Undergraduate)

  • Doctor of Medicine (MD)

  • Bachelor of Pharmacy (B.Pharm)

  • Bachelor of Science in Nursing Education

  • Bachelor of Science in Nursing

  • Bachelor of Medical Laboratory Sciences (BMLS)

  • Bachelor of Science in Medical Imaging & Radiotherapy

 Programu za Uzamili (Masters & PhD)

  • Master of Public Health (MPH)

  • Master of Medicine (MMed) kwa fani mbalimbali za tiba

  • Master of Science in Clinical Microbiology & Diagnostic Molecular Biology

  • Master of Science in Epidemiology & Biostatistics

  • Doctor of Philosophy (PhD) katika nyanja mbalimbali za afya na utafiti.

SOMA HII :  Sokoine University of Agriculture (SUA)

 Sifa za Kujiunga na Chuo

Ili kujiunga na kozi za CUHAS, wanahitaji kukidhi vigezo vya kila programu:

 Kwa Shahada ya Kwanza

✔ Kwa Doctor of Medicine au Shahada nyingine – lazima uwe na angalau passes tatu za msingi (principal passes) katika Fizikia, Kemia na Biolojia (na pointi inayokubalika) kutoka ACSEE.

✔ Kwa baadhi ya Shahada kama BSc Nursing au BMLS, unaweza pia kuhitaji daraja ya chini kama C/D kulingana na programu na mwongozo wa chuo.

✔ Waombaji waliomaliza Diploma katika taaluma husika wanaweza kuomba kama “equivalent entry” ikiwa GPA yao ni ya kutosha.

 Kwa Programu za Uzamili na PhD

✔ Waombaji wa uzamili wanahitaji shahada ya kwanza kutoka chuo kinachotambulika.
✔ Kwa PhD, unahitaji shahada ya uzamili kwa utafiti na uwezo wa kufanya kazi ya utafiti.

 Kiwango cha Ada

Ada za CUHAS hutofautiana kulingana na ngazi ya kozi, utaalamu na uraia wa mwanafunzi (wa ndani au wa nje). Kwa mfano programu za shahada ya kwanza kama MD, B.Pharm au BSc zinakuwa na ada tofauti kulingana na mzunguko wa masomo na mahitaji ya vitendo.
Kwa maelezo kamili ya ada, inashauriwa kuangalia prospectus rasmi au kuulizia ofisi ya udahili ya CUHAS, kwani ada zinaweza kubadilika kila mwaka.

Fomu za Kujiunga na Chuo / Jinsi ya Kuomba (Apply)

CUHAS ina mfumo wa maombi mtandaoni kupitia portal yao ya OSIM (Online Student Information Management System). Kwa kufanya hivyo:

  1. Tembelea https://osim.bugando.ac.tz/

  2. au sehemu ya maombi ya CUHAS. osim.cuhas.ac.tz

  3. Chagua daraja na kozi unayotaka kuomba.

  4. Jaza maelezo yako ya kibinafsi na kitaaluma.

  5. Ambatanisha nyaraka muhimu kama result slip, vyeti, na picha.

  6. Lipia ada ya maombi kupitia mfumo kama inavyoelekezwa.
     Kwa baadhi ya kozi, lazima ulipe application fee (kiasi hutofautiana kulingana na programu).

SOMA HII :  Chuo cha Ualimu Butimba Teachers College Online Applications

Students Portal / Mfumo wa Wanafunzi

CUHAS inatumia platform ya OSIM (Online Student Information Management) ambayo wanafunzi waliopo na waombaji wanaweza kutumia kufuatilia:

  • Hali ya maombi

  • Kupata barua za udahili

  • Kupata ratiba

  • Kusajili kozi

  • Kuangalia matokeo kama imewekwa portal

  • Malipo na taarifa nyingine za masomo.

 Tovuti rasmi ya portal ni https://osim.bugando.ac.tz/

 Jinsi ya Kuangalia Majina ya Waliochaguliwa

Majina ya waliochaguliwa kwa mwaka wa masomo hupatikana kwa njia zifuatazo:

  1. Ingia kwenye portal ya OSIM – Tazama sehemu ya “Application Status” au “Selected Applicants.”

  2. Chuo pia huweka tangazo la waliochaguliwa kwenye tovuti rasmi au kupakia orodha kama PDF kwa programu mbalimbali kama udahili wa diploma 2025/26.

  3. Angalia barua pepe yako mara kwa mara kwa taarifa rasmi kutoka chuo. osim.cuhas.ac.tz

Mawasiliano ya Chuo

Ikiwa unahitaji msaada zaidi kwa maswali ya udahili, kozi, ada au maelezo mengine, wasiliana na CUHAS kupitia:

 Anuani:
Catholic University of Health and Allied Sciences
Wurzburg Road, Bugando Medical Centre (BMC) Premises,
P.O. Box 1464, Mwanza, Tanzania

 Simu:
+255 28 298 3384
 Barua Pepe: vc@bugando.ac.tz

 Tovuti Rasmi:
www.bugando.ac.tz

About Burhoney 4809 Articles
Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika Ulimwengu wa Blogin ,Na Uandishi wa Makala Mbalimbali mitandaoni katika kuhakikisha nakuletea kilichobora nimekuwa nikitumia muda Wangu mwingi kujifunza juu ya mabadiliko ili kuendana na wakati